
Kikosi cha Yanga leo kinashuka dimbani kucheza mchezo wa ligi kuu soka ya Tanzania Bara TPL dhidi ya timu ya Ruvu Shooting inayotokea Mlandizi mkoani Pwani.
Yanga inashuka Dimbani ikiwa imetoka kupoteza mchezo wao uliopita dhidi ya Biashara United kutoka mkoani Mara.
Kuelekea mchezo huo klabu ya Yanga imethibitisha kuwakosa wachezaji wake Gadiel Michael , Mohammed Issa Banka ambao ni majeruhi na pia itamkosa mchezaji Andrew Vincent Dante ambaye anatumikia adhabu ya kadi tatu za njano.
Yanga pia itakuwa na furaha kwa nahodha wake Ibrahim AJibu kurejea kwenye kikosi cha timu hiyo baada ya kukosekana kwenye mchezo uliopita.
from sokoa news http://bit.ly/2LQibto
1

0 Comments