LIVE: Yanga 1-0 Zesco United, Ligi ya Mabingwa Barani Afrika


MAPUMZIKO: YANGA 1-0 ZESCO UNITED

Dak ya 45, Banka anapewa kadi ya njano kwa kucheza madhambi dhidi ya mchezaji wa Zesco, dakika moja imeongezwa kuelekea mapumziko.

Dak ya 43, kwa namna timu zote mbili zinavyocheza kila mmoja ana uwezo wa kupata matokeo licha Yanga kuwa inaongoza.
Dak ya 42, jaribio jingine wanalipata yanga lakini mawasiliano ya yanakuwa si mazuri, wanashindwa kulitumia.
Dak ya 37, Zesco wanafanya mabadiliko, anaingia Wiston Kalengo na anatoka Enock.
Dak ya 32, Zesco wanaonekana kutulia zaidi kwa sasa wakisaka bao la kusawazisha, wanajaribu kutafuta nafasi ya kufunga bao.
Dak ya 29, Yanga wanazidi kupata moto sasa, wanashambulia lango la Zesco kama nyuki.
Dak ya 24, Gooooooli, Sibomana anafunga penati yake kwa umaridadi kabisa, sasa Yanga wako mbele kwa bao 1-0.
Dak ya 23, penatiiiii, Yanga wanapata penati baada ya Sibomana kufanyiwa madhambi eneo la hatari, ni faida kwa Yanga. Anaenda kupiga Sibomana mwenyewe.

Dak ya 21, kosakosa nyingine imetokea kwenye lango la Zesco, inakuwa faulo na Mwamuzi anaamuru mpira upigwe kuelekea Yanga.
Dak 20, Zesco wanaonekana kutawala zaidi eneo la kati wakiwazidi Yanga japo kuipenya ngome ya wapinzani wao imekuwa ngumu.
Dak ya 19, Mpira unatoka nje na unakuwa wa kurushwa kuelekezwa lango la Zesco, tayari usharushwa.
Dak ya 18, Mnata anakuwa shujaa kwa mara nyingine tena, anaokoa shuti ambalo lingeweza kuwa msala kwake na Yanga.
Dak ya 15, Sibomanaaaaaa, anapiga kichwa kufuatia krosi safi ya Tshishimbi lakini inakwenda nje, ilikuwa nafasi nzuri sana kwa Yanga kaundika bao.

Dak ya 14, Zesco wanapata kona ya kwanza, wanapiga na inaleta hatari pale, Mnata anadaka, wanaanza upya.
Dak ya 11, Balamaaa anapiga shuti moja kaliii lakini linakwenda sentimita chache kulia kushoto mwa lango la Zesco.
Dak ya 10, Mnata anadaka mpira mwingine uliotokana na shambulizi kutoka kwa Zesco, kushoto mwa Uwanja.
Dak ya 7, shambulizi jingine wanafanya Zesco lakini uimara wa Mnata unasaidia, anaanzisha upya.
Dak ya 6, Fei Toto naye anapata nafasi ya kujaribu kufunga lakini anapiga mpira nje, ni golikiki.

Dak ya 5, Kamusoko anapata nafasi na anapiga shuti kali lakini uimara wa Mnata unamfanya adake kwa umaridaidi kabisa.
Dak ya 5, Mnatana anaonekana akipaza sauti kuwahamasisha wachezaji wenzake ndani ya uwanja wapambane.
Dak ya 4, Yanga wanajaribu shambulizi la kwanza ambalo linamfikia kipa wa Zesco na wao wanaanza upya.
Dak ya 3, Balama anatuliza  mpira kulia mwa uwanja, nyuma kidogo ya lango lake, anapia pasi kwenda mbele.
Dak ya 1, tayari mechi imeshaanza katika uwanja wa Taifa.

The post LIVE: Yanga 1-0 Zesco United, Ligi ya Mabingwa Barani Afrika appeared first on Global Publishers.




from sokoa news https://ift.tt/2ZZvv4j
1

Post a Comment

0 Comments