Yanga haitashiriki kombe la Kagame



Uongozi wa klabu ya Yanga umekataa mualiko wa kushiriki michuano ya kombe la Kagame inayofanyika mwezi ujao nchini Rwanda

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Yanga mapema leo, uongozi wa timu hiyo umesema idadi kubwa ya wachezaji wake wamemaliza mikataba

Aidha, taarifa hiyo imesema wachezaji wapya waliosajiliwa na timu hiyo baadhi bado hawajakamilisha taratibu za usajili huku wengine wakiwa wanakabiliwa na michuano ya Afcon

Pia taarifa hiyo imeongeza kuwa wachezaji wengine wenye mikataba wameruhusiwa kwenda likizo

Yanga ilialikwa kushiriki michuano hiyo mwaka huu ikiungana na Simba na Azam fc kutoka Tanzania

Simba pia imejitoa, Azam Fc mabingwa watetezi wamethibitisha watashiriki


from sokoa news http://bit.ly/2Zm31hn
1

Post a Comment

0 Comments