Ufaransa: Waandamanaji waendelea kumpinga Macron

Maandamano ya kupinga kupanda kwa bei za bidhaa mahitaji na ughali wa maisha yaendelea nchini Ufarasa.

Waandamanaji wamekuwa wakipinga kupanda kwa bei za bidhaa mahitaji nchini Ufaransa kwa wiki 34 sasa.

Wananchi walianza kuingia mitaani mnamo mwezi Oktoba wakimpinga Macron kutokana na hali mbaya ya uchumi nchini humo.

Watu zaidi ya 25000 wameripotiwa kushiriki katika maandamano hayo kote nchini Ufaransa.

Mjini Paris maandamano yameonekana kupamba moto zaidi.

Tangu kuanza kwa maandamano hayo idadi kubwa ya watu wamejeruhiwa.


from sokoa news https://ift.tt/2FXp2M4
1

Post a Comment

0 Comments